Ni nani mkali zaidi kati ya Lionel Messi, Radamel Falcao, na Alvaro Morata?

Radamel Falcao, Alvaro Morata, Lionel Messi and Paul Dybala
Radamel Falcao, Alvaro Morata, Lionel Messi na Paul Dybala
Huku wachezaji watatu wakiwa wamefunga mabao sita kwenye mechi 6, mbio za kushindania kiatu cha dhahabu zinaashiria kuwa zitakuwa mbio kali sana.
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero, kijana mpya wa Chelsea Alvaro Morata na Romelu Lukaku wa Manchester United wako kileleni kwa ufungaji wa mabao.
Lakini wako katika kiwango kipi na mawiji wengine wa Ulaya?
Wale wanaowania kiatu cha dhahabu barani Ulaya
Ni mwezi wa pili wa msimu na wachezaji wawili tayari wamefunga mabao kumi na zaidi.
Mshambuliaji wa Monaco Radamel Falcaoa, amefunga mabao 11 katika mechi saba za Ligue 1, huku Paulo Dybala, akiifunga Juventus mabao 10 kwenye mechi sita za Serie A.
Kwenye La Liga, Lionel Messi anaongoza kwa ufungaji kwa mabao tisa katika mechi sita.
Wafungaji bora ulaya hadi sasa msimu huu
MchezajiMechi zilizochezwamabaoDakika zilizochezwaDakika kwa kila bao
Paulo Dybala (Juventus)61046647
Radamel Falcao (Monaco)71157352
Lionel Messi (Barcelona)6954060
Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund)6853567
Ciro Immobile (Lazio)6854068
Edin Dzeko (Roma)5643172
Robert Lewandowski (Bayern Munich)6751574
Dries Mertens (Napoli)6645676
Alvaro Morata (Chelsea)6645776
Sergio Aguero (Man City)6646778
Edinson Cavani (PSG)7760887
Mauro Icardi (Inter)6653489
Romelu Lukaku (Man Utd)6654090

Ince, Redmond... Ronaldo?

Cristiano RonaldoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCristiano Ronaldo (katikati)
Cristiano Ronaldo wa Real Madrid, Tom Ince wa Huddersfield na Nathan Redmond wa Southampton wana kipi kwa pamoja?
Wote wako kwenye kikosi cha wacahwa wanlioana matyzuaia makuwna wangai wa uigumngaji wa mabao
Redmond alipiga mikwaju 21 katika mechi sita bila kufunga bao.
Ronaldo haonekani kufurahishwa na kasi ya Messi na matatizo yake ya kufunga mabao yanaendelea.
Nohodha huyo wa kikosi cha Ureno hajafunga bao hata moja msimu huu licha kujaribu mara 18 ,12 yakiwa kwenye mechi moja.
Ni nani mkali zaidi kati ya Lionel Messi, Radamel Falcao, na Alvaro Morata? Ni nani mkali zaidi kati ya Lionel Messi, Radamel Falcao, na Alvaro Morata? Reviewed by EXUPER ASSOCIATION on 21:30 Rating: 5

Post Comments

Powered by Blogger.